Vyakula Vitano Ambavyo Vinaimarisha Afya Yako.

Sehemu kubwa ya magonjwa yanayotusumbua zama hizi yanatokana na mfumo wetu wa maisha. Magonjwa kama kisukari, presha ya kupanda na hata kansa yanatokana na mfumo wa maisha tunayoishi.

Vyakula tunavyokula, vitu tunavyokunywa na mtindo wa maisha tunaoendesha vimekuwa chanzo kikubwa cha magonjwa haya yanayosumbua watu wengi kwa sasa.

Ili kujikinga na magonjwa haya, kuna baadhi ya vitu unavyohitaji kubadili kwenye maisha yako. Leo tutajadili vyakula vitano ambavyo ukijenga tabia ya kuvitumia utajikinga na maginjwa mengi sana. Uzuri wa vyakula hivi ni kwamba vinapatikana kwa urahisi na havina gharama kubwa.

1. Nafaka ambazo hazijakobolewa.

Utumiaji wa nafaka ambazo hazijakobolewa unapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo. Pia nafaka hizi zinaondoa sumu kwenye mwili.

nafaka

2. Bisi(Popcorn).

Huenda umekuwa ukiziona bisi na kufikiri ni chakula cha watoto. Bisi zina virutubisho vinavyoitwa polyphenols ambavyo vinapambana na seli zinazosababisha kansa.

popcorn

3. Mayai.

Mayai yana virutubisho vinavyoitwa lutein ambavyo vinaondoa sumu mwilini. Virutubisho hivi vinaweza kuyalinda macho yako na upofu.

mayai

4. Maharage.

Maharage yana virutubisho vingi ambavyo vinaondoa sumu mwilini.

maharage

5. Sukari asili.

Vyakula vyenye sukari asili kama asali na sukari guru vina virutubisho vinavyoondoa sumu kwenye mwili.

asali

Fanya mabadiliko katika vyakula unavyokula ili uweze kuimarisha afya yako.

Kwa ushauri zaidi wa kiafya andika email kwenda afya@kisimachamaarifa.co.tz

0 comments: