Sababu 5 Kwa Nini Ni Marufuku Wewe Kukata Tamaa.

Katika maisha kuna wakati ambapo mambo huwa magumu sana. Ni katika nyakati hizi ambapo watu wengi hukata tamaa na kuacha kile ambacho walikuwa wanafanya.

Kwa kukata tamaa unashindwa kufikia mafanikio na pia unaona maisha yako kama hayana maana.

Leo JIONGEZE na sababu hizi tano kwa nini ni marufuku wewe kukata tamaa.

1. Bado hujafa.

Kama bado unaishi hii ina maana kwamba kila kitu kinawezekana. Hata iwe umeshindwa au kupoteza kiasi gani, jipange tena na utafikia mafanikio.

2. Kuna watu wengine walishafanya.

Katika jambo lolote ambalo linakushinda kufanya, kuna watu wengine walipitia changamoto kama zako ila waliweza kufikia mafanikio. Na kwa bahati nzuri sana watu hawa wameandika yote hayo kwenye vitabu, vitafute na uvisome.

3. Kuna watu wana hali mbaya kuliko wewe.

Wakati wewe unalalamika huna viatu kuna mwenzako hana miguu kabisa. Hivyo kukata tamaa na wakati kuna watu wana matatizo makubwa kuliko wewe na bado wanaishi utakuwa hujitendei haki.

USIKATE TAMAA2

4. Utawahamasisha wengine.

Kama ukiweza kufikia mafanikio licha ya changamoto unazokutana nazo utawahamasisha wengine nao kuweza kufikia mafanikio. Kama utakata tamaa na kuacha utawakatisha na wengine tamaa na kuwafanya wasijaribu kabisa.

5. Unastahili kuwa na furaha.

Kila mmoja wetu anastahili kuwa na furaha kwa sababu furaha hupewi na mtu bali inatoka ndani yako. Unapokata tamaa huwezi kuwa na furaha, badala yake utaona maisha yako kuwa kisirani. Ila kama utakomaa na kufanikiwa utakuwa na furaha idumuyo.

Sasa umeshajiongeza na sababu hizi tano za kutokata tamaa. Endelea kukomaa na utafikia mafanikio makubwa. Kama mambo yanazidi kuwa magumu badilisha mbinu ila sio kuacha kufanya kabisa.

Nakutakia kila la kheri.

0 comments: