Biashara 5 Unazoweza Kuanza Kufanya Bila Ya Kuwa Na Mtaji.

Kikwazo kikubwa cha watu wengi kuingia kwenye biashara kimekuwa ni mtaji. Japo sio kweli kwamba mtaji pekee ndio kikwazo, lakini wengi wanaamini mtaji tu ndio unawazuia.

Lakini pia wakati huo ambao mtu hana mtaji hakuna juhudi kubwa anazofanya ili kuhakikisha anapata mtaji huo.

Sasa kufupisha habari leo JIONGEZE na biashara hizi tano unazoweza kuanza kuzifanya bila ya kuanza na mtaji wa fedha.

1. Biashara ya mtandao(Network marketing).

Hii ni biashara ambayo ni mkombozi kwa mtu yeyote ambaye ana kiu ya kufikia mafaniki. Hapa tanzania kuna makampuni mengi yanayofanya biashara hii kamA Forever living, Oriflame, GNLD, na mengineyo. Katika makampuni haya kuna ambayo unaweza kuanza na kiasi cha chini sana ambacho ni sawa na bure.

2. Biashara ya ushauri.

Je kuna kitu ambacho una utaalamu nacho? Je kuna kitu ambacho unapenda sana kukifuatilia na hivyo unakijua sana? Vizuri, kuna mtu anataka kukijua ila hajui aanzie wapi. Kwa wewe kutoa ujuzi na uzoefu wako unaweza kulipwa fedha.

3. Biashara ya taarifa(internet marketing).

Hii ni biashara ya kutoa taarifa kwa kupitia mtandao wa intanet. Unaweza kuwa na blog yako ambayo ni bure kuiendesha na baadae ukaanza kupata kipato kizuri kupitia mtandao.

Soma; jinsi ya kutengeneza fedha kwa kutumia mtandao wa intaneti.

4. Biashara ya uwakala wa mauzo(salesman.)

Kuna makampuni mbalimbali ambayo yanatumia mawakala kuuza bidhaa au huduma zao. Kwa wewe kujifunza na kuwa wakala wao unaweza kupata kipato kizuri kwa njia ya kamisheni.

5. Biashara ya udalali.

Hii ni biashara ambayo wewe unamsaidia mtu kupata kitu anachotaka na hana muda au uzoefu wa kukipata. Kama ukiweza kuifanya biashara hii kwa mbinu nzuri unaweza kutengeneza kipato kizuri.

Angalizo; Biashara hizi zinahitaji wewe ufanye kazi kwa bidii na maarifa na pia unaweza usione faida mapema. Ila ukiweka malengo na mipango mizuri utaona mafanikio makubwa baadae.

Uzuri ni kwamba unaweza kuanza biashara hizi ukiwa bado umeajiriwa au upo masomoni.

Nakutakia kila la kheri.

TUKO PAMOJA.

0 comments: