JE WAJUA? Kuhusu Bacteria Wanaoishi Kwenye Kinywa Chako.
Kuna bacteria wengi wanaoishi kwenye kinywa chako zaidi ya idadi wa watu wanaoishi duniani.
Bacteria pia wapo kwenye ngozi yako, utumbo mpana na hata sehemu ya uke.
Kwa bahati nzuri bacteria hawa hawana madhara na wapo hapo kukukinga na bacteria wabaya.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA
Sasa unajua kwamba sio bacteria wote wanaoishi kwenye mwili wako ni hatari.
9/29/2014 12:53:00 PM | Labels: JE WAJUA? | 0 Comments
Mambo Matano Ya Kushangaza Kuhusu Siku Ya Jumatatu
Jumatatu ni siku ya kwanza ya wiki. Ni siku ambayo watu wanatoka kwenye mapumzimko na kuanza tena wiki ya kazi. Na kwa kuwa watu wengi hawapendi kazi wanazofanya, jumatatu inaonekana kuwa siku mbaya sana.
Haya ni mambo matano ya kushangaza ambayo hutokea sana siku za jumatatu tofauti na siku nyingine za wiki.
1. Zaidi ya asilimia 50 ya wafanyakazi huchelewa kazini.
Tafiti nyingi zinaonesha jumatatu ndio siku ambayo inaongoza kwa watu kuchelewa kufika kazini au kuwa watoro kazini.
SOMA; Mambo matano ya kufanya siku ya jumatatu ili uwe na wiki yenye mafanikio.
2. Asilimia kubwa ya watu hujiua.
Tafiti zilizofanywa hasa kwenye nchi zilizoendelea zinaonesha kwamba jumatatu ndio siku ambayo inaongoza kwa watu kujiua.
3. Asilimia kubwa ya watu hupata shambulio la moyo.
Jumatatu ndio siku ambayo watu wengi hupata shambulio la moyo(heart attack) zaidi ukilinganisha na siku nyingine za wiki. Hii inaweza kusababishwa na shinikizo kubwa la damu kutokana na kurejea kwenye kazi.
4. Mvua hainyeshi sana.
Inasemekana siku za jumatatu haina mvua sana ukilinganisha na siku nyingine za wiki. Hii inatokana na kwamba mwisho wa wiki watu wengi hawafanyi kazi na hivyo hakuna uchafuzi mkubwa.
5. Ni siku nzuri ya kununua gari.
Jumatatu ni siku nzuri ya kununua gari kwani wauzaji wa magari wanakuwa wameuza sana mwishoni mwa wiki na hawategemei wateja wengi siku ya jumatatu hivyo kuwa tayari kupunguza bei kwa kiasi kikubwa.
Nakutakia jumatatu njema na epuka mambo yanayoweza kukuharibia maisha yako hasa yanayotokea siku za jumatatu.
Tuko pamoja.
9/29/2014 08:20:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kuupuuza Ukweli.
I've learned that to ignore the facts does not change the facts.
Nimejifunza kwamba kuupuuza ukweli haibadilishi ukweli.
Ukweli ni ukweli hata kama utaamua kuupuuza. Kubaliana na ukweli na angalia jinsi ya kuutumia kupata kile unachotaka.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.
9/29/2014 06:52:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kuanza Upya.
Though no one can go back and make a brand new start, anyone can start from now and make a brand new ending.
Japokuwa hakuna anayeweza kurudi nyuma na kuanza upya, mtu yoyote anaweza kuanza sasa na kuwa na kesho nzuri.
Usikatishwe tamaa na makosa uliyofanya nyuma, anza leo kufanya yale yatakayokuwezesha kufikia mafanikio makubwa.
TUKO PAMOJA.
9/27/2014 10:04:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
JE WAJUA? Mambo Kumi Usiyojua Kuhusu Kupumua.
1. Mtu mzima anapumua mara 23,000 kwa siku.
2. Kazi kubwa ya kupumua sio kupata oxygen, bali kuondoa kabon dayoksaidi.
3. Kupumua kwa kutumia mdomo ni hatari kwa afya yako.
4. Unavyopumua kwa kasi ndivyo inavyozidisha njaa na acid kwenye mwili wako.
5. Unatakiwa kufanya mazoezi kwa kiwango ambacho utaweza kupumua ukiwa umefunga mdomo.
6. Pua ina ngazi nne za kuchuja hewa inayoingia, ukipumua kwa mdogo unenda moja kwa moja kwenye ngazi ya nne.
7. Kama mapafu yako yangetandazwa yanafiki ukubwa wa uwanja wa tennis.
8. Kupumua kunaendeshwa na mfumo wa fahamu usio wa hiari(involuntary).
9. Ukijizuia kupumua unaongeza kabon dayoksaidi kwenye mwili.
10. Ukijizuia kupumua unatibu kwi kwi.
Sasa umeshajua mambo muhimu kuhusu kupumua, pumua vyema.
Nakutakia kila la kheri.
9/26/2014 03:09:00 PM | Labels: JE WAJUA? | 0 Comments
Ushauri Kwa Wajasiriamali Kutoka Kwa Mwanzilishi Wa Facebook.
Mmoja wa waanzilishi wa Facebook Dustin Moskovitz, ambaye amekuwa bilionea kupitia kampuni hiyo, sasa anamiliki kampuni nyingine inayotoa ushauri kwa wajasiriamali na wanaotaka kuingia kwenye ujasiriamali.
Anasema tofauti na vyombo vya habari vinavyoonesha kwamba ujasiriamali ni kitu cha ufahari na rahisi, ni kazi ngumu sana ambayo inahitaji ujitoe sana.
Anasema hivi ndivyo vyombo vya habari vinavyoaminisha watu ujasiriamali ukoje;
Na hivi ndivyo uhalisia ulivyo;
Na hapa ametoa ushauri wa vitabu sita ambavyo kila mjasiriamali au anayepanga kuingia kwenye ujasiriamali ni muhimu kuvisoma;
Tafuta vitabu hivyo na uvisome, vitakusaidia katika safari yako ya ujasiriamali.
Nakutakia kila la kheri, TUPO PAMOJA.
9/26/2014 07:50:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kinachokurudisha Nyuma.
It's not who you are that keep's you back, it's who you think you're not. So start believing in yourself!
Kinachokurudisha nyuma sio vile unavyofikiri upo bali vile unavyofikiri haupo. Anza kujiamini sasa na amaini unaweza kufanya mambo makubwa.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.
9/26/2014 07:36:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Mambo 10 Unayotakiwa Kujua Kuhusu Uwekezaji.
Moja ya njia za kuelekea kwenye utajiri ni kuwa mwekezaji. Unapokuwa mwajiriwa unawasaidia wengine kuwa matajiri. Unapojiajiri au kufanya biashara unaanza kujijengea utajiri. Unapokuwa mwekezaji unakuwa kwenye nafasi kubwa ya kufikia utajiri.
Hivyo ni muhimu sana wewe kuwa mwekezaji. Ila kabla hujawa mwekezaji, JIONGEZE na mambo haya kumi muhimu unayotakiwa kujua kuhusu uwekezaji.
1. Akiba uliyoweka benki sio uwekezaji. Hela iliyoko benki inazalisha kiasi kidogo sana na wakiondoa makato ni kama hakuna unachopata. Hata ukiwa na nyingi kiasi gani benki, sio uwekezaji.
2. Uwekezaji ndio njia pekee ya kuenda na mfumuko wa bei. Ukiweka hela benki, inapungua thamani kutokana na mfumuko wa bei. Ukiwekeza hela thamani yake inaongezeka jinsi mfumuko wa bei unavoongezeka.
3. Uwekezaji ni hatari. Kupitia uwekezaji unaweza kutengeneza fedha nyingi na pia unaweza kupoteza fedha nyingi.
4. Kununua hisa ni kumiliki kampuni. Unaponunua hisa za kampuni fulani unakuwa unamiliki sehemu ya kampuni hiyo. Ikipata faida na wewe unapata na ikipata hasara na wewe unapata.
5. Vipande ni kukopesha fedha. Unaponunua vipande ni kama umeikopesha taasisi fedha na hivyo kuweza kuitumia kwenye shughuli nyingine za kibiashara. Baadae unapata faida kutokana na vipande vyako.
6. Kuanza mapema ni faida kubwa. Kama utaanza kuwekeza ukiwa na umri mdogo ukifikia uzeeni utakuwa umefaidika sana na umejifunza sana.
7. Uwekezaji maarufu sio mzuri kwako. Kitu ambacho ni maarufu sana na ambacho kila mtu anawekeza hakina faida kubwa.
8. Usiwekeze fedha utakayoihitaji karibuni. Uwekezaji una changamoto nyingi sana na kama thamani imeshuka sana ukisubiri itapanda tena. Kama unawekeza fedha ambayo unatarajia kuitoa huwezi kunufaika.
9. Hakuna awezaye kutabiri soko la kesho. Ni vigumu sana kuweza kutabiri ni nini kitatokea siku zijazo, lakini unaweza kujipanga vizuri.
10. Unahitaji kujifunza kila siku kuhusu uwekezaji na mbinu mbali mbali za mafanikio kwenye uwekezaji. Soma kitabu THE INTELIGENT INVESTOR, utajifunza mengi.
Anza sasa kuwekeza au kuweka mipango ya kuwekeza. Jinsi utakavyoanza mapema ndivyo utakavyonufaika zaidi. Kwa hapa tanzania unaweza kuwekeza kwa kununua hisa, kununua vipande vya UTT, kununua ardhi, Kujenga nyumba za kuuza na kupangisha na hata kununua kampuni au biashara.
Nakutakia kila la kheri, TUPO PAMOJA.
9/25/2014 07:30:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kushinda Vikwazo Kwenye Maisha.
Nobody trips over mountains. It is the small pebble that causes you to stumble. Pass all the pebbles in your path and you will find you have crossed the mountain.
Hakuna mtu anayeuvuka mlima kwa hatua moja. Ni mawe madogo madogo ndio yanayokuzuia. Yavuke mawe yote kwenye njia yako na utajikuta umeshauvuka mlima.
Tatizo lolote kubwa linalokukabili linaweza kutatulika vizuri sana kama utaligawa katika sehemu ndogo ndogo.
Nakutakia kila la kheri.
9/25/2014 07:05:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Ukiacha Kuangalia Facebook Kila Mara Mambo Haya Matano Yatatokea.
Facebook ni mtandao mkubwa sana wa kijamii ambao unaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi. Facebook imekuwezesha kujuana na watu wengi, kukutana na marafiki mliopotezana zamani na hata kujifunza mambo mengi. Hata makala hi unaweza kuwa umeipata kupitia facebok.
Pamoja na faida hizi, facebook imekuwa chanzo kikubwa cha watu wengi kupoteza muda kwani ina utegemezo mkubwa. Unaweza kujikuta kila siku unaangalia ni nini kinaendele kwenye facebook.
Kama utaacha kuangalia facebook kila mara, mambo haya matano yatatokea.
1. Utaacha kufa akili.
Kila mara unapotumia facebook ni kama akili yako inakuwa imekufa. Kwa sababu unajikuta akili yako yote imeingia kwenye mtandao huo na hivyo kushindwa kuona na kufikiria mambo mengine yanayoendelea. Kwa mfano unaweza kuwa umepanda gari safari nzima uko kwenye facebook tu na hivyo kushindwa kuona vitu vingine ambavyo vingekufanya ufikiri zaidi.
2. Utakamilisha kazi nyingi.
Kila mara unapoingia facebook hasa kwenye kuda wa kazi ni kama unajiibia muda wako wa kazi. Hivyo ukiweza kujidhibiti na ukapunguza muda unaoingia kwenye mtandao huu utakamilisha kazi nyingi.
3. Utawajua marafiki zako wa kweli ni kina nani.
Kupata marafiki kwenye mtandao ni rahisi sana. Unaweza kulike post zao au kuweka maoni kila mara na tayari mkawa karibu. Ila urafiki wa ukweli unahitaji zaidi ya hapo. Hivyo punguza muda unaotumia kwenye mtandao na ujue marafiki zako wa kweli ni watu gani.
4. Utaacha kujilinganisha na wengine na hivyo kujikubali.
Facebook inaweza kuwa sehemu ya kukufanya uone hakuna unachofanya cha maana. Hii inatokana na kuona wengine wakifanya mambo makubwa. Wakati mwingine unachokiona sio kweli.
SOMA; HIvi ndivyo mitandao ya kijamii inaharibu akili yako, kuwa makini.
5. Utagundua ulikuwa unatumika kibiashara.
Facebook zamani ilikuwa nzuri sana ila kwa sasa hivi wanatumia taarifa zako kuwauzia watu wa matangazo. Hivyo kila utakapoingia utakutana na matangazo na post nyingi za marafiki zako hutaziona tena. Kwa njia hii facebook wanakutumia wewe kibiashara.
Tumia mitandao ya jamii lakini usikubali mitandao hii ikutumie wewe.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.
9/24/2014 12:58:00 PM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Sehemu Tano Unazoweza Kupata Mtaji Wa Kuanzia Biashara.
Kisingizio kikubwa cha watu kushindwa kuanza biashara kimekuwa ni mtaji. Kila siku watu wanalalamika wanapenda kuanza biashara ila mtaji hawana. Lakini wakati huo hawafanyi jitihada zozote za kupata mtaji huo au kuanza kidogo na kufikia makubwa.
Kulalamika kwamba taasisi za fedha hazitoi mkopo kwa watu ambao hawana dhamana ni kupoteza muda wako. Nikuulize wewe akija mtu yeyote akakuambia nipe elfu kumi nitakurudishia nikiipata utampa? Ni vigumu sana. Kwa kuwa ni vigumu kupata mkopo kwenye taasisi za fedha leo JIONGEZE na sehemu hizi tano ambazo unaweza kupata mtaji wa kuanzia biashara.
1. Akiba zako mwenyewe.
Kama huna kazi ya kukupatia kipato tafuta hata kazi ya kibarua, ifanye na weka akibakatika kila unachopata, baada ya muda tumia akiba hii kuanza biashara.
2. Michango kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki.
Unaweza kukusanya mchango kutoka kwa ndugu jamaa na hata marafiki. Wape wazo lako na omba wakuchangie.
3. Kuanza na biashara ambayo haihitaji mtaji.
Kuna biashara nyingi ambazo unaweza kuanza bila ya mtaji. Anza na biashara hizi na ukishaanza kupata kipato kikubwa unaweza kuhamia kwenye biashara unayoitaka.
SOMA; Biashara tano unazoweza kuanza kufanya bila mtaji.
4. Kuandaa wazo zuri.
Kama una wazo zuri sana ambalo linaweza kufanyika ila huna mtaji, liandae wazo hilo vizuri sana na kisha angalia kampuni ambazo zinaweza kufaidika na wazo hilo kisha wauzie wazo hilo au wakupe sehemu ya faida itakayopatikana kwa wazo lako.
ANGALIZO; Sajili wazo lako kwenye mamlaka husika(BRELA) ili usije ukaibiwa wazo hilo.
5. Shiriki mashindano mbalimbali.
Kuna mashindano mengi sana yanafanyika siku hizi ambayo yanapambanisha mawazo bora ya kibiashara. Andaa wazo lako na ingia kwenye mashindano haya. Ukiweka wazo lako vizuri unaweza kuwa mshindi na ukapata mtaji.
Tumia njia hizo tano kupata mtaji wa kuanzia biashara. Kama unaona njia hizi hazifai au haziwezekani kwako endelea kukaa nyumbani na kuperuzi mitandao ya kijamii huku ukiendelea kupoteza muda.
Amua sasa kubadili maisha yako, chukua hatua.
9/24/2014 11:00:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kufikia MAFANIKIO MAKUBWA.
The greatest oak was once a little nut that held its ground!
Mti unaaonekana mkubwa siku moja ulikuwa mbegu ambayo ilishikilia ardhi.
Shilikia misingi yako na siku moja utafikia mafanikio makubwa. Usiyumbishwe wala kukata tamaa.
TUPO PAMOJA.
9/24/2014 09:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Mambo Matano(5) Ambayo Ni Marufuku Kufanya Kwenye Eneo La Kazi.
Kazi ndio msingi wa maendeleo. Na ili uweze kufikia mafanikio makubwa ni lazima ufanye kazi kwa bidii na maarifa. Sifa moja kubwa ya kufanikiwa kwenye kazi yoyote ni kupenda unachofanya. Kuna mambo mengi sana ambayo ukiyafanya kwenye kazi yako yanakuzuia kufikia mafanikio.
Leo JIONGEZE mambo haya matano ambayo ni marufuku kuyafanya eneo la kazi kama unataka kufikia mafanikio makubwa.
1. Kuonesha tabia ya hasira au kulipiza kisasi.
Mara kwa mara mtapishana kauli na mfanyakazi wako, mfanyakazi mwenzako au bosi wako. Kwa vyovyote vile tafuta njia ya kumaliza tofauti zenu kwa amani, ukiongea au kufanya mambo kwa hasira au kupanga kulipiza kisasi utaingia kwenye matatizo makubwa.
2. Majungu na kusengenya.
Maeneo mengi ya kazi hapa Tanza ia kuna majungu mengi sana. Usianzishe wala usishiriki kumpiga jungu mtu yeyote aliyepo kwenye eneo lako la kazi. Ni kumkosea heshima na hii itakufanya uingie kwenye matatizo.
3. Kudanganya.
Wafanyakazi wengi wamezoea kudanganya hapa na pale. Tatizo kubwa la kudanganya kwenye eneo lako la kazi ni kwamba itakubidi uishi uongo huo kwa muda mrefu kitu ambacho kitakuumiza.
4. Kuchukua sifa za wengine.
Kuna watu wanasubiri wengine wafanye kazi halafu wao ndio wanaokuwa wa kwanza kusema kama sio mimi hiki kisingewezekana. Usifanye hivi, utakosa ushirikiano kutoka kwa wengine. Kila mtu ana nafasi kubwa kwenye kukamilika kwa jambo lolote.
5. Usichome daraja.
Watu wengi wanaojiajiri wanatokea kwenye ajira. Zamani kidogo watu walikuwa wakiondoka kwenye ajira zao kwa ugomvi mkubwa na hivyo kuondoa kabisa ushirikiano. Wewe usifanye hivi, kama unakwenda kujiajiri hakikisha unakuwa na uhusiano mzuri na mwajiri wako kwani anaweza baadae kuwa mteja wako au akakuletea wateja. Mafanikio ya sasa yanatokana na ushirikiano mzuri uliojenga na watu.
Epuka kufanya mambi hayo matano kwenye kazi yako kama kweli unataka kupata mafanikio kupitia kazi hiyo.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.
9/24/2014 06:50:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Watu Watatu(3) Waliofukuzwa Kwenye Kampuni Walizoanzisha Wenyewe.
Unaweza kufikiri kuingia kwenye biashara na kujiajiri mwenyewe ndio njia nzuri ya wewe kuwa na uhuru kwa kile unachofanya. Inaweza isiwe kweli kwa sababu kwa jinsi hali ya biashara za kisasa ilivyo unaweza kujikuta kwenye hali ngumu sana.
Tena pale unapofikia kampuni ikawa kubwa na kuanza kuuza hisa, wenye hisa nyingi wanaweza kufanya maamuzi hata ya kukufukuza wewe japo wewe ndiye uliyeanzisha.
Hapa ni orodha ya watu watatu ambao walifukuzwa kwenye kampuni walizoanzisha wenyewe;
1. Steve Jobs, Apple
Steve Jobs alianzisha kampuni ya apple ila baadae alifukuzwa kwenye kampuni hiyo. Alikuja kurudishwa kwenye kampuni hiyo na kuleta mapinduzi makubwa ya kiteknolojia.
2. Ted Tunner, CNN
Ted Tunner alianzisha CNN, shirika la habari la marekani lakini baadae alikuja kufukuzwa kwenye shirika hilo.
3. Jack Dorsey, Twitter
Jack Dorsey ni mmoja wa waanzilishi wa mtandao wa kijamii unaoitwa twitter ila kwa sasa anaonekana hayupo tena kwenye mtandao huo kwani ameanzisha kampuni nyingine ya teknolojia.
Kuwa makini pale unapoanzisha kampuni yako yasije kukutokea mambo ambayo hukutarajia.
Nakutakia kila la kheri.
9/23/2014 11:00:00 AM | Labels: NILICHOJIFUNZA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Lifti Ya Kuelekea Kwenye Mafanikio.
There is no elevator to success. You have to take the stairs.
Hakuna lifti ya kuelekea kwenye mafanikio, ni lazima upande ngazi.
Watu wengi wamekuwa wakidanganywa sana kwamba kuna njia ya kupata mafanikio haraka, kama vile mtu anavyopanda lifti na kufika ghorofa ya kumi haraka.
Ukweli ni kwamba hakuna njia yoyote inayoweza kukuletea mafanikio haraka. Kama ilivyo kwamba itakuchukua muda kupanda ngazi mpaka ufike ghorofa ya kumi.
Usikate tamaa, SONGA MBELE.
9/23/2014 09:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 1 Comments