Mambo Matano Ambayo Watu Waliofanikiwa Hufanya Mwisho Wa Wiki.
Kwa taratibu nyingi za kazi kwa walioajiriwa na hata aliojiajiri mwisho wa wiki huwa ni siku za mapumziko. Kwa walioajiriwa wanaweza kuwa na siku mbili za mapumziko na waliojiajiri wanaweza kuwa na muda mfupi zaidi ya hapo.
Jinsi unavyoweza kutumia siku hizo za mwisho wa wiki inaweza kukufanya ufikie mafanikio au ushindwe kufikia mafanikio.
Hapa utaona mambo matano ambayo watu wenye mafanikio makubwa hufanya mwisho wa wiki.
1. Hupumzika.
Japokuwa siku hizi ni za mapumziko bado sio watu wote wanapumzika. Wengine hutumia muda huu kufanya kazi nyingine zaidi. Watu wenye mafanikio hupata muda wa kupumzika mwisho wa wiki.
2. Hufanya tathmini wa wiki inayoisha.
Watu wenye mafanikio hutenga muda mwisho wa wiki na kufanya tathmini ya wiki inayoisha. Huangalia ni kipi walishofanikiwa na ni wapi waliposhindwa.
3. Hupanga wiki inayoanza.
Watu wenye mafanikio hutumia mwisho wa wiki kuweka malengo na mipango ya wiki inayofuatia. Mipango hii huwawezesha kuwa na wiki yenye mafanikio makubwa.
4. Hujumuika na ndugu na jamaa.
Watu wengi wenye mafanikio huwa na kazi nyingi sana katikati ya wiki na hivyo kukosa nafasi ya kuonana na ndugu jamaa na marafiki. Hutumia mwisho wa wiki kujumuika na watu ambao hawajakuwa nao kwa muda mrefu.
5. Hukata mawasiliano.
Watu wenye mafanikio hutenga masaa machache mwisho wa wiki kukata mawasiliano yote. Hutumia muda huu kukaa na kutafakari maisha yao zaidi. Katika kukata mawasiliano huondoka kwenye mtandao, huzima simu na vifaa vingine vyote vya mawasiliano.
Na wewe unaweza kufanya mambo haya kila mwisho wa wiki na ukaboresha maisha yako zaidi.
Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.
9/20/2014 01:23:00 PM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kufikia Ndoto Zako.
If you are facing in the right direction, all you have to do is keep on walking in order to reach your dreams.
Kama upo kwenye uelekeo sahihi, unachotakiwa kufanya ni kuendelea na safari ili kufikia ndoto zako.
Ukishachagua njia yako usirudi tena nyuma, endelea kukaza mwendo ili uweze kufikia malengo yako.
TUKO PAMOJA.
9/20/2014 12:47:00 PM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Hivi Ndivyo Mitandao Ya Kijamii Inavyoharibu Akili Yako, Kuwa Makini.
Tunaweza kukubali kwamba mitandao ya kijamii ndio mapinduzi ya sasa. Yaani kama ilivyokuwa mapinduzi ya viwanda, sasa tuna mapinduzi ya mitandao ya kijamii. Mitandao kama facebook, twitter, instagram, linked in na mingine mengi imekuwa sehemu ya maisha yetu.
Mitandao hii imekuwa na faida kubwa sana, kuwaleta watu karibu zaidi ya ilivyowahi kutokea. Watu wengi wamefahamiana kupitia mitandao hii na wengine wanatengeneza kipato kupitia mitandao hii.
Kama tunavyojua, chochote chenye faida huwa kina hasara. Leo tutaangalia hasara ya mitandao ya kijamii kwenye akili yako na hivyo kuharibu maisha yako.
Kwenye mitandao hii ya kijamii kwa mfano facebook au instagram, watu huweka picha zao mbalimbali wakiwa katika hali ya furaha au kustarehe. Kupitia picha hizi kama na wewe hujapata nafasi ya kuwa katika hali hizo unaweza kuona maisha yako sio mazuri kama ya wale ambao wanaweka picha nzuri.
Kwa mfano mtu anaweka picha anakula vyakula vizuri anakuandikia I AM HAVING LUNCH, wakati huo wewe unakula makande au wali maharage ni manyanyaso makubwa sana kisaikolojia. Hali kama hii inakufanya wewe ujione maisha yako sio mazuri kama ya watu hao.
Kitu unachotakiwa kukumbuka ni kwamba watu hawa wameweka picha hizo nzuri chache tu, kuna siku wanakula makande kama wewe ila hawaleti picha zao kwenye mitandao. Kuna siku wanashinda njaa ila hawatakuandikia kwamba wameshinda njaa.
Hivyo acha kujilinganisha na chochote unachokiona kwenye mtandao wa kijamii. Kama mtu kaweka picha anakula vizuri au kavaa vizuri au yuko kwenye kiwanja kizuri usijaribu kujilinganisha hata kidogo. Maisha yako wewe yanaweza kuwa bora kuliko hata ya watu hao.
Tumia mitandao ya kijamii kujumuika na wengine ila isiwe sehemu ya wewe kujilinganisha na wengine na hatimaye kuona maisha yako hayana thamani.
TUKO PAMOJA.
9/20/2014 11:50:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 2 Comments
Faida Tano Za Muziki Kiafya Na Mziki Mzuri Unaoweza Kusikiliza Leo.
Watu wengi wanapenda kusikiliza mziki ili kuburudika, ila mziki una faida nyingi sana ukiacha kuburudika tu.
Mziki una faida kiafya kwa yeyote anayesikiliza. Ila mziki tunaozungumzia hapa ni mziki laini.
Zifuatazo ni faida tano za mziki kiafya.
1. Mziki husaidia hupunguza maumivu.
Watu ambao wanateseka na maumivu makali wameonesha kupata afadhali wanaposikiliza muziki laini.
2. Mziki unaimarisha kinga ya mwili.
Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasayansi zinaonesha kwamba kusikiliza muziki kunaimarisha kinga ya mwili.
3. Mziki unawasaidia watoto njiti.
Watoto njiti ambao wamezaliwa kabla ya muda wa kawaida wa mtoto kuzaliwa wanaweza kunufaika sana na mziki uliopangiliwa vizuri na unaoendana na sauti zilizopo kwenye tumbo la mama.
4. Mziki unasaidia wazee.
Wazee mara nyingi hujisikia wapweke na kuwa na sononeko. Kwa kusikiliza mziki wanapata ahueni kwa kipindi kidogo.
5. Mziki unaweza kukusaidia kupunguza huzuni.
Kama una huzuni au umekasirishwa ukisikiliza mziki laini hasira zako zinaweza kupungua kwa kiasi kikubwa.
Anza kusikiliza mziki laini sasa na upate faida hizo na nyingine nyingi kiafya. Unaweza kuanza kwa kusikiliza mziki huo hapo chini.
9/20/2014 08:57:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
PICHA; Nchi Zilizotawaliwa Na Uingereza Na Miaka Zilipopata Uhuru.
9/19/2014 06:28:00 PM | Labels: NILICHOJIFUNZA LEO | 0 Comments
NILICHOJIFUNZA LEO; Sababu Za Kihistoria Kwa Nini Scotland Ilitaka Kujitenga Na Uingereza.
Jana tarehe 18/09/2014 wananchi wa Scotland walipiga kura ya kuamua kama Scotland ijitenge na kuwa na mamlaka yake kamili au iendelee kuwa sehemu ya Uingereza(United Kingdoms). Matokeo ya kura hiyo yaliyotangazwa leo asubuhi yanaonesha kwamba asilimia 55.3 wamekataa kujitenga na asilimia 44.7 walipiga kura ya kutaka kujitenga. Kwa matokeo hayo Scotland inaendelea kuwa sehemu ya Uingereza.
Nilitaka kujifunza zaidi juu ya muungano huu wa Scotland na England.
Mwaka 1602 malkia Elizabert I wa England alifariki dunia bila ya kuacha uongozi kwa watu wa familia yake. Mfalme James I wa Scotland alikuwa msimamizi wa ncho zote mbili lakini kila nchi ilikuwa na uhuru wake.
Mwaka 1707 viongozi wa Scotland walikubali kuungana moja kwa moja na England kutengeneza United Kingdoms. Baadhi ya wananchi wa Scotland hawakufurahishwa na maamuzi haya ni hivyo yalitokea maandamano mengi kupinga muungano huo. Kwa miaka mingi baadhi ya wananchi wa Scotland wamekuwa wanajaribu kujitoa ila wanashindwa.
Mwaka 1999 Scotland waliweza kuwa na bunge lao. Uingereza waliruhusu Scotland kuweza kufanya maamuzi yao juu ya mambo kama afya, nyumba na elimu, lakini bajeti walipangiwa na Uingereza.
Bado wananchi wengi wa Scotland hawakufurahishwa na hili na hivyo manunguniko ya chini chini yalikuwa yakiendelea. Chama cha upinzani kiliposhika nafasi ya kuongoza bunge la Scotland viongozi wake walipendekeza ipingwe kura ya kuamua kuendelea kuwepo chini ya Uingereza au kujitegemea wenyewe.
Haya yote ndiyo yaliyopelekea kwenye kura iliyofanyika jana. Na kama tulivyoona kwenye matokeo asilimia 44 ya wanaotaka kujitenga sio ndogo na hivyo huenda chokochoko zikaendelea.
Tunaweza kujifunza nini hapa kwenye muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar? Karibu kwa maoni.
9/19/2014 04:09:00 PM | Labels: NILICHOJIFUNZA LEO | 0 Comments
Faida Tano (5) Za Kulala(Kusinzia) Mchana.
Katika jamii zetu kulala mchana inaweza kuonekana kama uvivu. Yaani mtu anayelala mchana anaonekana ni mvivu na hapendi kazi. Kinyume na imani hii kulala mchana kuna faida kubwa sana kuliko ulivyowahi kufikiri.
Leo utajifunza faida tano za kulala mchana na kama utaweza uweke ratiba hiyo kwenye kila siku yako.
1. Inapunguza stress.
Kufanya kazi kwa siku nzima inaweza kukufanya uwe na stress nyingi sana. Kupata dakika chache za kulala inapunguza stress hizi.
2. Inaongeza uwezo wa kujifunza na kumbukumbu.
Ni rahisi sana kujifunza na kukumbuka yale uliyojifunza kama akili inakuwa imepumzishwa. Kulala mchana kunaipumzisha akili.
3. Inaongeza ubunifu.
Kama unafanya kazi ambazo zinahitaji ubunifu wa hali ya juu kuwa na utaratibu wa kulala mchana na unapoamka unakuwa katika nafasi nzuri ya ubunifu.
4. Ni bora kwa afya yako.
Tafiti zinaonesha kwamba watu wanaolala mchana wanauwezekano mdogo wa kupata magonjwa ya moyo ukilinganisha na ambao hawalali mchana.
5. Inaongeza ufanisi.
Watu ambao wanalala mchana huamka wakiwa na ufanisi mkubwa kuliko ambao wanafanya kazi siku nzima.
Ni muda gani ulale?
Muda wa wewe kulala mchana ni mfupi sana kati ya dakika 20 mpaka 25. Hivyo hata kama unafanya kazi unaweza kutenga dakika 20 baada ya chakula na ukasinzia au kulala kidogo. Sio lazima ulale kitandani, hata kkuinamisha kichwa chako kwenye meza inakutosha kunufaika na usingizi huo. Anza sasa kujilaza dakika 20 na uboreshe maisha yako.
Nakutakia kila la kheri.
9/19/2014 02:42:00 PM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Muonekano Wako Wa Nje.
How things look on the outside of us depends on how things are on the inside of us.
Jinsi mambo yanavyoonekana kwa nje inategemea na jinsi tulivyo ndani yetu.
Anza kubadili kilichoko ndani yako ili kuona mabadiliko ya nje. Anza na mawazo yako, ukibadili mawazo yako utaona mabadiliko kwa nje.
Nakutakia siku njema.
9/19/2014 09:01:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Uerevu
A wise man does in the beginning, what a foolish man does in the end.
Mtu mwerevu hufanya mwanzoni, kile ambacho mpumbavu hufanya mwishoni.
Kuwa mwerevu sasa kwa kujifunza kupitia makosa ya wengine na usiyarudie.
Nakutakia kila la kheri.
9/18/2014 01:14:00 PM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Mambo 10 Unayotakiwa Kuacha Kufanya Ili kuboresha Maisha Yako.
Maisha yetu ya kila siku yana changamoto nyingi sana. Lakini sehemu kubwa ya changamoto hizi tunasababisha wenyewe kutokana na maamuzi tunayofanya au tabia zetu wenyewe.
Hapa kuna mambo kumi ambayo unatakiwa uache kuyafanya ili uweze kuwa na maisha bora.
1. Acha kulalamika sana kwenye maisha yako. Kulalamika hakutakusaida zaidi ya kukufanya ujione huna msaada. Kama kuna kitu hukipendi kibadilishe, kama huwezi kukibadilisha achana nacho.
2. Acha kujiongezea msongo wa mawazo. Usijipe kazi nyingi kupiata uwezo wako, usiahidi mambo mengi na usijaribu kufanya kila kitu.
3. Acha kujutia makosa uliyofanya zamani. Kuendelea kujutia kila siku na kukumbuka ulichopoteza au ulichokosa hakutakusaidia chochote zaidi ya kukuumiza. Jifunze kutokana na makosa hayo na songa mbele.
4. Acha kuhofia kesho yako na anza kufanyia kazi ndoto zako. Hofu ni kitu ambacho hakipo ila kinakuzuia wewe kufikia mafanikio makubwa. Achana na hofu sasa na fanya kitu kufikia ndoto zako.
5. Acha kusogeza mambo mbele na anza leo. Umesema unataka kuanza biashara ila utaanza kesho, kesho haitafika, anza leo kuweka mipango yako na anza kuifanyia kazi.
6. Acha kutegemea watu wengine ndio wakupe furaha, kumbuka furaha inatoka ndani yako.
7. Acha kulinganisha maisha yako na ya watu wengine. Hakuna mtu mwenye uwezo ambao unao wewe. Kazana kuwa bora kila siku ila sio kujilinganisha na wengine.
8. Acha kusubiri muda muafaka. Unasubiri muda muafaka ndio uanze biashara? Muda muafana ndio sasa, hutapata muda mwingine mzuri kama huu kufanya kile ambacho unataka kufanya.
9. Acha kukimbia matatizo yako. Kukimbia matatizo sio kuyasuluhisha, yataendeleakukufata ulipo. Yakabili matatizo yako na uyatatue.
10. Acha kukaa na watu wanaokurudisha nyuma. Watu unaokaa nao wana ushawishi mkubwa sana kwako. Kama unakaa na watu waliokata tamaa na wanaolalamika tu na wewe utakuwa hivyo hivyo.
Boresha maisha yako kwa kuacha kufanya mambo haya ambayo yanakurudisha nyuma.
TUKO PAMOJA.
9/18/2014 09:18:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Fanya Mambo Haya Matano Kila Siku Asubuhi Na Utakuwa Na Siku Yenye Mafanikio.
Kila siku inayoanza ni siku mpya kwako kuleta mabadiliko kwenye maisha yako na dunia kwa ujumla. Hijalishi siku ya jana ilikuwaje kwako, ila leo unayo kwenye mikono yako na ni uamuzi wako kama unataka kuifanya siku yenye mafanikio au unataka kuipoteza.
Fanya mambo haya matano kila siku asubuhi na utakuwa na siku yenye mafanikio makubwa.
1. Amka asubuhi na mapema. Unapoamka asubuhi na mapema unakuwa na faida ya kuwa macho kabla ya watu wengine. Muda huu ni muda wenye utulivu na unaweza kufanya mambo yako vizuri.
2. Soma nusu saa kila siku. Baada ya kuamka mapema, tumia nusu saa ya kwanza akujisomea kitabu kizuri kitakachokufundisha na kukuhamasisha. Kama huna kitabu bonyeza hapa na uweke email yako utatumiwa vitabu.
3. Pangilia siku yako. Andika ni mambo gani matatu ambayo ukiyakamilisha siku ya leo yatakuletea mafanikio makubwa. Pangilia jinsi utakavyofanya mambo hayo.
4. Fanya mazoezi. Unapofanya mazoezi asubuhi unauweka mwili wako katika hali ya uchangamfu na ukakamavu, hata akili yako inaweza kufanya kazi vizuri.
SOMA; Faida 5 za kukimbia dakika 5 kila siku.
5. Pata kifungua kinywa. Ni muhimu sana kupata kifungua kinywa asubuhi. Hii ni kwa sababu unapolala ni kama unakuwa umefunga na hivyo unapoamka mwili unakuwa hauna chakula cha kutosha.
Haya ni mambo ambayo unaweza kuanza kuyafanya mara moja na ukaona mabadiliko kwenye maisha yako. Hebu anza kuyafanya sasa na upate mafanikio kwneye maisha yako.
TUKO PAMOJA.
9/18/2014 07:14:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Mambo Matano(5) Ya Kufanya Wakati Unaelekea Kukata Tamaa.
Maisha yana changamoto nyingi sana. Kuna wakati mambo yanaweza kuwa magumu sana kwako na kuona kama vile huo ndio mwisho wa dunia. Huu ndio wakati ambao unakata tamaa na kuona haiwezekani tena. Kabla ya kufikia hali hii ya kukata tamaa kuna mambo matano ya kufanya ambayo yatabadili kabisa hali yako.
1. Pitia tena malengo yako. Ni kipi hasa kinakusukuma ufanye hicho unachofanya? Ni nini hasa kinakufanya utake kufikia malengo hayo. Ukijua sababu hii itakusukuma zaidi hata mambo yanapokuwa magumu.
2. Kumbuka mafanikio yako. Kabla hujakata tamaa hebu kumbuka ni mambo mangapi umeshafanikiwa mpaka sasa. Kama unafikiri hujafanikiwa kwa lolote, fikiri tena kwa kina.
3. Kumbuka kwamba vikwazo ni sehemu ya maisha. Hakuna safari ya maisha iliyonyooka, kila mtu aliyefikia mafanikio makubwa alikutana na vikwazo vikubwa sana.
4. Fanya kile unachoweza kufanya kwa ubora. Wakati mambo yanapokuwa magumu badala ya kutumia muda mwingi kufikiria kwa nini mambo yanakwenda hivyo, tumia muda wako kufanya kile unachoweza kufanya kwa ubora wa hali ya juu. Utaongeza thamani na kuweza kuondoka kwenye magumu.
5. Kumbuka kwamba hauko peke yako. Kuna watu wengi sana ambao wako tayari kukusaidia katika hali unayopitia. Moja ya njia rahisi za kupata msaada wa watu hawa ni kusoma vitabu vya kukuhamasisha. Kuna vitabu vingi sana vinavyoweza kukuhamasisha na kubadili kabisa mtazamo wako. Soma nusu saa kila siku na utaona mabadiliko makubwa. Kama huna kitabu cha kusoma bonyeza hapa na uweke email yako utatumiwa vitabu.
Fanya mambo haya machache unapokuwa unapitia hali ngumu yenye kukatisha tamaa. Kumbuka ya kwamba kama utakata tamaa ndio unakuwa umeaga mashindano. Ila kama ukiendelea kuvumilia utaibuka mshindi.
Nakutakia kila la kheri.
9/17/2014 03:35:00 PM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Uwezo Wako Mkubwa.
If you think you are too small to be effective, you have never been in the dark with a mosquito!
Kama unafikiri wewe ni mdogo sana kuweza kuleta mabadiliko makubwa, hujawahi kukaa kwenye giza ukiwa na mbu.
Kila mmoja wetu ana uwezo mkubwa ulioko ndani yake. Ujue uwezo wako na utumie kufikia mafanikio makubwa.
TUKO PAMOJA.
9/17/2014 01:22:00 PM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
Faida 5 Za Kukimbia Dakika 5 Kila Siku.
Kila mtu anafahamu kwamba mazoezi ni kitu muhimu sana kwa afya njema na maisha kwa ujumla. Lakini inapokuja kwenye kufanya mazoezi, watu wengi hufikiri ni lazima kwenda kwenye eneo maalumu la mazoezi au kununua vifaa maalumu. Kwa hiyo ukosefu wa vifaa hivyo na ukosefu wa muda pia hufanya watu wengi kushindwa kufanya mazoezi.
Leo utajifunza faida tano za kukimbia dakika tano kila siku. Nani ambaye hana dakika tano kwenye siku yake? Nani ambaye hana eneo la kukimbia dakika tano? Jibu ni hakuna.
Hizi ndio faida 5 za kukimbia dakika 5 kila siku.
1. Inapunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo. Magonjwa ya moyo sasa hivi yamekuwa tishio sana kutokana na watu kutofanya mazoezi.
2. Utaishi muda mrefu. Kwa kufanya mazoezi utakuwa na afya imara na hivyo utaweza kuishi muda mrefu zaidi.
3. Inakusaidia kuwa katika hali nzuri. Kwa kufanya mazoezi unakuwa katika hali nzuri inayokuwezesha kufanya majukumu yako kwa ufanisi zaidi.
4. Unapata usingizi mzuri. Kwa kufanya mazoezi, mwili unapata nafasi nzuri ya kupumzika unapolala, na hivyo kuwa na usingizi mzuri.
5. Kuongeza ufanisi wa akili. Mazoezi hasa yanapofanywa asubuhi huifanya akili kuwa katika ufanisi wa hali ya juu.
Hizi ndio faida tano unazoweza kuzipata kwa kukimbia dakika tano kila siku. Anza leo jioni au kesho asubuhi ili kuepuka magonjwa na pia kuongeza ufanisi wa akili yako.
TUKO PAMOJA.
9/17/2014 10:02:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Mbinu 5 Zitakazokufanya Uwe Mbunifu Zaidi.
Iwe umeajiriwa au umejiajiri unalipwa kulingana na ubunifu wako. Kama unataka kulipwa zaidi, yaani kupata wateja wengi zaidi au kupata kipato kikubwa zaidi ni muhimu kila siku kuongeza ubunifu wako kwenye kile unachofanya.
Hizi hapa ni mbinu tano zitakazokufanya uwe mbunifu zaidi;
1. Pata muda wa kupumzika. Tafiti zinaonesha kwamba mtu anapokuwa amechoka, uwezo wake wa kufikiri unakuwa chini sana.
2. Fikiria kama mtoto. Watoto wana ubunifu mkubwa sana kwa sababu hufikiri bila ya kujiwekea mipanga. Anza kuondoa mipaka kwenye fikra zako na ufikiri kwa uhuru zaidi.
3. Fanya mazoezi. Mazoezi ni muhimu sana ili kuweka akili yako katika ufanisi wa hali ya juu.
4. Jipe muda wa mwisho wa kukamilisha kitu. Kama kuna jukumu unafanya jipe muda ambao ni lazima uwe umemaliza. Jinsi muda unavyokaribia kuisha utajikuta unapata mawazo mazuri ya kufanya.
5. Usikatae mawazo mabaya haraka. Wakati unafikiri unaweza kuja na mawazo mengi sana. Usianze kujiwekea mipaka kwamba hili ni zuri na hili ni baya, yaangalie yote vizuri na ujue ni kipi cha kufanya.
Tumia mbinu hizi kila siku na utaona ubunifu wako ukiongezeka.
Muhimu; Kila siku fanya unachofanya kwa ubunifu zaidi.
TUKO PAMOJA.
9/17/2014 07:31:00 AM | Labels: MBINU ZA MAISHA | 0 Comments