Maswali 12 Muhimu Ya Kujiuliza Ili Kuweza Kufikia Mafanikio.

Mafanikio ni kitu ambacho kila mtu anakazana kukifikia. Japokuwa kila mmoja wetu ana maana yake ya mafanikio, kila mmoja kuna kitu ambacho anapifana kukipata kwenye maisha yake.

Kitu hiki ambacho kila mmoja wetu anakipigania sio rahisi kupatikana. Ndio maana kuna watu wengi wanahangaika lakini bado wanaishia kukata tamaa.

Leo hapa UTAJIONGEZA na maswali kumi na mbili muhimu ya kujiuliza ili uweze kufikia mafanikio kwenye jambo lolote unalofanya.

Jiulize na kujijibu maswali haya ili uweze kujua unaelekea wapi. Ingekuwa vizuri zaidi kama majibu yako utayaandika kwenye karatasi.

1. Ni kitu gani ninachotaka kwenye maisha?

2. Ni yapo machaguo yangu?

3. Ni dhana gani ambayo unatengeneza?

4. Nina majukumu gani?

5. Ninawezaje kufikiria tofauti na ninavyofikiri sasa?

6. Watu wengine wanafikirije kwa jambo hili ninalofikiri mimi?

7. Ni kitu gani ambacho nimejifunza kutokana na makosa ambayo nimewahi kufanya?

8. Ni kitu kitu gani ninachokosa au ninachokwepa?

9. Ni hatua gani ninazoweza kuchukua ili kuelekea kule ninakotaka?

10. Ni maswali gani muhimu nayotakiwa kuendelea kujiuliza na pia kuuliza wengine?

11. Nawezaje kubadili hali mbaya ninayopitia ili kuwa nzuri na kufaidika nayo?

12. Ni kitu gani kinawezekana?

Jiulize maswali hayo mara kwa mara kila wakati ambapo unakutana na changamoto au kikwazo na hata pale unapoweka malengo mapya.

0 comments: